Changamoto na vikwazo vya Maisha

Posted by Apolinary Macha on 18:30 with No comments


"Jifunze kutazama changamoto za maisha katika mtazamo tofauti"

Vikwazo na changamoto mbalimbali katika maisha ni hali ambayo huwepo kwa kila mtu. Ukitazama dunia kwa upande mwingine au kwa upande wa uhalisia utagundua kuwa kila kiumbe, vitu, wanadamu n.k vinapata changamoto fulani.

Chukulia mfano wa ukuaji wa mbegu: Mbegu inapoanza kuota na kukua hupitia changamoto mbalimbali. Lakini cha ajabu kupitia changamoto hizo mbegu hutumia changamoto hizo kujiboresha na kujiimarisha na hatimaye mbegu huota, hukua na kuzaa mbegu nyingine ambazo nazo zinapitia changamoto hizo.

Hebu jiulize, maisha yangekuwa hayana changamoto ungeimarika?
Changamoto hukupa nafasi ya kujipima, kutazama vitu katika hali tofauti ambayo bila changamoto usingeona hivyo, husaidia kujua njia za kuepuka changamoto hizo na kukuimarisha katika ubunifu wa maisha. 

BADALA YA KUACHIA CHANGAMOTO ZA MAISHA ZIKUTESE, TUMIA NAFASI HIYO KUJIIMARISHA.