Kufikia malengo ya mbali, kunaaza na malengo haya haya madogo tuliyonayo kwa sasa.

Posted by Apolinary Macha on 12:13 with No comments


Watu wengi wamekuwa na mawazo na malengo yanayofanana: 
“Kufanya mambo makubwa maishani, kufanya shughuli zenye manufaa kwenye jamii, mafanikio, pesa, familia, mali n.k.”

Pia kutokana na malengo haya utakuta kuna anayewaza
“Nikiwa CEO, nitafanya maamuzi yenye manufaa kwenye kampuni”
“Nikiwa na Biashara nitatenga fungu kidogo kusaidia watu”

Hivyo tunaishi maisha yetu tukiwa tunatamani kuwa katika hali mbalimbali ili kufanya mambo yenye manufaa kwenye jamii. 

Lakini mtazamo huu ni mzuri, japo una changamoto zake. Kwa maana ya kwamba, tunakuwa na mawazo kuwa mpaka uwe fulani…ndio utafanya mambo fulani… hali hii inatusahaulisha kuwa hata kwa muda huu ambao upo katika hatua yoyote bado unaweza kufanya mambo makubwa kama vile ambapo ungekuja kuwa hapo baadae. 

“Usisubiri kuwa CEO ndio uwe unafanya maamuzi ya msingi kwenye kampuni, usisubiri uwe na pesa ndio usaidie wenye shida, usisubiri uwe na pesa ndio uanze kufanya mazoezi, unaweza kuanza chochote hata sasa katika nafasi hii hii uliyonayo." 

Katika maisha, mambo madogo tunayoyafanya ndio msingi mkubwa katika maisha yetu. Furaha ni matokeo ya juhudi ndogondogo unazofanya katika maisha yako kila siku. Kila hatu uliyopo unaweza kufanya jambo dogo na kwa ukubwa. Pengine bado unapendelea kuwa na mambo makubwa, lakini kumbuka hata katika hali hii ndogo unaweza kufanya mambo yaliyo na msingi kabla ya kusema usubiri mpaka baadae ndio utaanza kuyafanya. Chochote unachofanya sasa kina msingi mkubwa katika maisha yako. Ukiwa na uelewa hii utazoea kufanya jambo wakati wowote, kwa hali yoyote na kwa ukubwa kutokana na kujenga mazoea sahihi mapema.