Tumia Fikra kidogo na hisia zaidi.

Posted by Apolinary Macha on 15:27 with 2 comments

Osho quote Osho Swahili
Toka nje ya kichwa chako na ingia kwenye moyo wako, fikiria kidogo na ongeza hisia Zaidi – Osho

Ulishawahi kushikiliwa na akili? Au mawazo yako? Mfano badala ya kuweza kusuluhisha tatizo au jambo lililopo akilini unashindwa na badala yake akili ndio inazidi kuzidisha matatizo?

Kuna watu husema kuwa unavyozidi kulifikiria jambo ndipo unazidisha mawazo juu ya jambo unalofikiria, kumbuka akili inapenda kuwaza, unapopeleka wazo lolote kwenye akili ndipo unazidisha tatizo na sio kusuluhisha. Akili itazidi kuunganisha matukio, kukuambia kuna hiki na hiki na siku zote fahamu kuwa akili ina hofu. Akili inaogopa lakini siku zote moyo hauogopi. Moyo hauwezi kujua hofu bali akili ndiyo inayotambua hofu. Unapoona una hofu juu ya jambo lolote sio moyo wako umeona hivyo bali ni akili/fikra yako ndio ipo hivyo.

Ni vyema badala ya kutumia akili sana kuwaza, tumia na moyo kuhisi. Ni vigumu sana kujua hisia ya moyo na siku zote unapojaribu kutaka kufahamu moyo unataka nini akili huwa inakuzuia na inaweza kukudanganya kuwa moyo unahisi hivi kumbe sio kweli.

Roho zetu ndio zinatuunganisha na malaika mlinzi wetu na Muumba wetu, ukisikiliza roho inataka nini ufahamu kuwa hiyo ndio sauti ya ndani ambayo inamwelekeza kila mmoja wetu.

Muda utakaoweza kuusikiliza moyo unataka nini na akili nayo itatulia na itauheshimu moyo na maamuzi yake. Kumbuka maamuzi yaliyotoka kwenye nafsi ni ya muhimu na kuzingatia. Hutusaidia kufanya maamuzi mazuri hata tusipotambua mbeleni kuna nini.
Categories: , ,